Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maalim Seif kukaribishwa rasmi Zanzibar, mamia wamiminika kumsikiliza

47811 SEIF+PIC

Thu, 21 Mar 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Unguja. Viongozi na wanachama wa ACT-Wazalendo wameanza kuwasili katika viwanja vya Vuga mjini Unguja kushiriki mkutano wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.

Machi 18, 2019 Maalim Seif alijiunga na ACT-Wazalendo na leo Alhamisi Machi 21, 2019, mwanachama huyo mpya anakaribishwa rasmi katika ofisi za chama hicho visiwani Zanzibar sambamba na kutoa neno kwa wananchi na viongozi wa chama chake hicho kipya.

Mwananchi lililopo katika viwanja hivyo limeshuhudia wananchi hao wakiwa wamevalia sare za chama hicho huku wakisubiri kumshuhudia na kumsikiliza Maalim Seif.

Ratiba iliyotolewa na chama hicho inaeleza kuwa mbali na mambo mengine, lengo kuu ni kumkaribisha Maalim Seif kwenye ofisi za ACT Zanzibar.

Kaimu Katibu Uenezi wa ACT Zanzibar Seif Hamad Suleiman, amesema kufanyika kwa mkutano huo hakuna maana ya kuanza mikutano ya hadhara bali ni kuwakaribisha wanachama wapya.

“Lengo si kuanza mikutano bali kuwakaribisha wageni ndani ya chama chetu,” amesema Suleiman.

 



Chanzo: mwananchi.co.tz