Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad ameifananisha vuta nikuvute inayoendelea kati ya polisi na viongozi wa chama hicho upande wa Profesa Ibrahim Lipumba kama mchezo wa kuigiza kwa jambo ambalo lipo wazi kuwa mkutano huo si halali.
Amesema jeshi la polisi likiamua lina uwezo mkubwa wa kuzuia mkutano huo unaoendelea jijini Dar es Salaam kutokana na zuio la mahakama lilitolewa kuhusu mchakato huo.
Soma zaidi: Polisi wazuia mkutano wa ‘CUF Lipumba’
Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne Machi 12, 2019, Maalim Seif amesema “Ni kama mchezo wa kuigiza kuhusu suala hili.”
“Kama polisi ina nia ya dhati ya kuzuia wale hawawezi kufanya lolote lile. Utafanyaje mkutano wakati kuna zuio tena la Mahakama Kuu? Amehoji Maalim Seif.
“Siyo mantiki yoyote kwa polisi kuanza kuzungumza na viongozi wa CUF wa upande ule wakati suala lipo wazi kabisa. Nawaambia msimamo wetu upo pale pale mkutano huu hatuutambui kabisa kwa sababu ni haramu,” amesema Maalim Seif.
Related Content
- VIDEO: ‘CUF Lipumba’ wakaidi agizo la Polisi, waendelea na mkutano
- Polisi wazuia mkutano wa ‘CUF Lipumba’
Soma zaidi: ‘CUF Lipumba’ wakaidi agizo la Polisi, waendelea na mkutano