Mon, 24 Aug 2020
Chanzo: zanzibar24.co.tz
Mwenyekiti wa TLP Augustino Mrema ameonyesha kusikitishwa na baadhi ya watu kuwatambua wagombea wawili tu Charles Kimei anayegombea Jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi, na James Mbatia anayegombea kupitia tiketi ya NCCR Mageuzi.
“Wagombea tupo saba, lakini inasikitisha wanaotajwa ni wawili tu, kwa nini? tutambueni na sisi wa vyama vingine,” amesema.
Mrema anaingia kwenye mchuano mkali wa kuwania Jimbo hilo kwa mara nyingine baada ya kuanguka kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 ambapo aliambulia kura 6,416 wakati Mbatia alibuka kidedea kwa kupata kura 60,187.
Chanzo: zanzibar24.co.tz