Mgombea wa urais Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama cha ACT WAZALENDO Bernard Membe amesema kuwa yeye ni mgombea halali wa chama hicho na hakuna mgombea mwengine wa urais.
Kaulihhio ameitoa wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo Membe amesema
“Mimi Bernard Membe ni mgombea halali wa ACT-Wazalendo wa nafasi ya Urais. Na chama chetu ni kizuri kabisa na nitaipeleka Oktoba 28, 2020 vizuri kabisa siku ya uchaguzi ili Watanzania wakaamue.” – Bernard Membe.
“Ombi langu kwa Serikali ya awamu ya tano, haki ya Mungu ikubali matokeo na ihakikishe haki inakuwepo. Hili ni pamoja na Zanzibar, tusiishie kusema amani, amani bila uwepo wa haki. Haki ni msingi wa amani.”