Mgombea wa Urais Zanzibar kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, ameahidi endapo akichaguliwa na kuwa rais basi atahakikisha wakulima wa viungo na karafuu wanakuwa huru kuuza mazao yao sehemu yoyote wanayotaka duniani.
Mgombea wa Urais Zanzibar kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, ameahidi endapo akichaguliwa na kuwa rais basi atahakikisha wakulima wa viungo na karafuu wanakuwa huru kuuza mazao yao sehemu yoyote wanayotaka duniani. Maalim Seif amesema kwenye utawala wake utawashauri wakulima wa bidhaa za viungo kujikita zaidi kwenye viungo ambavyo vitaleta tija za haraka kwao na Serikali kwa ujumla