Thu, 27 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu amesema ripoti ya Kikosi Kazi iliyokabidhiwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni, imejaza upungufu na kwamba imeiga mambo yaliyomo kwenye Rasimu ya Katiba ya Jaji Joseph Warioba.
“Taarifa hiyo inarudia kosa la tangu uhuru kuweka katiba mikononi mwa Rais, tangu mwaka 1962 katiba zetu zinalenga Rais anataka nini,” amesema Lissu.
“Wamependekeza Tume iendelee kutumia watumishi wa umma kwenye uchaguzi, tangu mwaka 1995 hawa watumishi wa umma ni watu wa CCM, na kikosi kazi kinasisitiza waendelee kuwa wasimamizi,” amesema Lissu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live