Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Lema: Millya alihama siku nyingi Chadema

21311 Lema+pic TanzaniaWeb

Tue, 9 Oct 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema aliyekuwa mbunge wa Simanjiro, James Millya alihama siku nyingi ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumapili Oktoba 7, 2018 muda mfupi baada ya barua ya Millya kusambaa kuwa amejizulu, Lema amesema hajashtuka wala kushangazwa na uamuzi huo wa kuamua kurejea CCM.

“Millya alikuwa ameshahama muda mrefu Chadema, ukiangalia matendo, mienendo yake, sisi tulishamwona amehama,” amesema.

Soma zaidi:Chadema washtushwa taarifa za Millya kujiuzulu

Lema ambaye amekiri ni rafiki wa Millya na alihusika katika kumpokea wakati akihamia Chadema mwaka 2013 amesema, “Kilichonishangaza ni Millya kuchelewa kwenda CCM. Millya alipaswa kuwa mtu wa kwanza kabla ya madiwani na wabunge kuhamia lakini amekuwa wa mwisho ndicho kinanishangaza.”

“Bado sijaelewa hao wanaosema wanakwenda kuunga mkono, utaungaje mkono juhudi kukiwa na matatizo mengi, demokrasia inafinyangwa, waandishi wanatekwa, watu wanapotea, uchumi mgumu, ajira ni tatizo,” alihoji Lema.

“Unapokuwa mwanasiasa wa upinzani unapaswa kujua unapigania si masilahi yako bali ya wajukuu na vizazi vijavyo lakini kwa Millya ameamua kujinufaisha yeye binafsi,” amesema.

 Soma zaidi: Mbunge wa saba upinzani ahamia CCM

 

 

Chanzo: mwananchi.co.tz