Fri, 3 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde 'Kibabaji' amesema ukame wa Dodoma haukuwa ukame wa hali ya hewa kwenye ardhi bali ulikuwa ukame wa mawazo wa kubadili changamoto kuwa fursa.
Akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Kibajaji amesema serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imewafumbua macho.
Kwa lipi? Anajibu kwamba Samia ameifanya Dodoma kuwa ardhi ya kilimo kwa kuanzisha mabwawa ya umwagiliaji, jambo ambalo limechochea uzalishaji katika mkoa huo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live