Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kilichojiri kikao cha halmashauri kuu ya CCM hiki hapa

64667 Ccm+pic

Thu, 27 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam.  Kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, kimewateua Omar Kumbilamoto na Geofrey Mwanichisye kugombea nafasi ya unaibu meya wa manispaa ya Ilala, Dar es Salaam na Mikindani Mtwara kupitia chama hicho.

Mbali na hilo kimewapendekeza Omary Zubeir Mbwana, Elizaberth Andrea Mihale na Abdulrahaman Makame Shake kugombea nafasi ya ujumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya mkoani Kaskazini Pemba visiwani Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Itikadi na Uenezi wa CCM , Hamphrey Polepole imeeleza kikao hicho kimefanyika leo Alhamisi Juni 27, 2019 Ikulu jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Mwenyekiti wake, Rais wa Tanzania John Magufuli.

Polepole amesema kikao hicho kiliwapendekeza Makame Omar Makame, Othman Ali Maulid na Suleiman Ame Vuai kugombea ujumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya mkoa wa Kusini Unguja.

“Kikao kiliwapendekeza Bakari Msangi, Gerald Munisi na Elipokea Urio kugombea nafasi ya katibu wa siasa na uenezi wa mkoa wa Arusha. Pia kikao kimeridhia kwa kauli moja pendekezo la Kamati Kuu la kumteua  Munde Tambwe (Mbunge wa Viti Maalum) kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa,” amesema Polepole.

Mbali na hilo, Polepole amesema kikao wajumbe wa kikao hicho wamepokea na kujadili taarifa ya uhakiki wa mali za chama hicho  uliofanyika Zanzibar na kuelekeza sekretarieti ya halmashauri kuu ya taifa kuchukua hatua stahiki za kinidhamu kwa waliohusika na kupeleka mashauri yao kwa kamati ndogo ya usalama, maadili na udhibiti wa nidhamu kwa wale wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine kuhujumu mali za chama.

Pia Soma

Taarifa hiyo imeeleza kikao hicho kimejadili na kupitisha kanuni za Chama Cha Mapinduzi katika maeneo ya;-  Kanuni za Utumishi za wafanyakazi wa CCM na Jumuia zake Toleo la 2019; Kanuni za Uteuzi wa Wagombea wa CCM katika vyombo vya Dola, Toleo la 2019; Taratibu za Sehemu ya Wazee, Toleo la 2019 na Kanuni ya Jumuia ya Umoja wa Vijana wa CCM, kuhusu Idara na Uteuzi wa Wakuu wa Idara.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz