Dar es Salaam. Nani mwingine ataondoka Chadema. Ndilo swali unaloweza kujiuliza kutokana na waliokuwa wanachama wa chama hicho kukikimbia kwa nyakati tofauti, tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa 2015.
Leo Jumanne Februari 18, 2020 aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji amehamia CCM na kupokewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho tawala, Dk Vicent Mashinji.
Mwaka 2020 umeanza vibaya kwa Chadema. imeshuhudiwa Waziri mkuu mstaafu, Frederick Sumaye akihama Chadema na kurejea CCM na juzi aliyekuwa mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe naye alirejea CCM.
Sumaye alijiunga Chadema mwaka 2015 akitokea CCM na Mwambe akifanya hivyo mwaka huohuo baada ya kutoswa katika kura za maoni ndani ya CCM akiwania ubunge wa Ndanda. Alipotua Chadema alipewa nafasi ya kugombea na kuibuka na ushindi.
Leo Dk Mashinji aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema kuanzia Februari 2016 hadi Desemba 2019, baada ya kupewa nafasi ya kuzungumza alieleza sababu za kukihama chama hicho kama zilizotolewa na Mwambe na Sumaye.
Swali la kujiuliza nani mwingine kung’oka Chadema, ni suala la muda tu.
Habari zinazohusiana na hii
- Dk Mashinji ahamia CCM
- VIDEO: Sumaye ataja sababu kurejea CCM
- VIDEO: Sumaye arejea CCM
- Cecil Mwambe arejea CCM