Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kauli ya Lijualikali baada ya kuhojiwa na TAKUKURU

LIJUAL Kauli ya Lijualikali baada ya kuhojiwa na TAKUKURU

Fri, 12 Jun 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mbunge wa Kilombero Peter Lijualikali, amewataka Wabunge wote ambao wameitwa na TAKUKURU kwa ajili ya mahojiano, waseme ukweli na si kudanganya.

Lijualikali ameyabainisha hayo leo Juni 11, 2020, mara baada ya kutoka kufanyiwa mahojiano na taasisi hiyo kufuatia tuhuma walizozitoa dhidi ya CHADEMA, kuwa walikuwa wanakatwa mishahara yao kila mwezi, ambapo Wabunge wa kuchaguliwa walikuwa wakikatwa laki 5, huku Wabunge wa Viti Maalum wao walikuwa wakikatwa Milion 1.5.

"Mahojiano yalikuwa mazuri na ya kirafiki, niwaombe wenzangu ambao wanakuja kwamba TAKUKURU imejipanga wana kila taarifa, yaani kama umejipanga kuja kudanganya, hauwezi kudanganya kabisa" amesema Lijualikali.

TAKUKURU Makao Makuu imesema kuwa itawahoji jumla ya Wabunge 69, pamoja na waliowahi kuwa Wabunge wa CHADEMA, ikiwa ni mwendelezo wa uchunguzi wa malalamiko dhidi ya matumizi ya fedha za chama zilizolalamikiwa na baadhi ya waliowahi kuwa Wabunge kupitia chama hicho.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live