Wed, 17 Oct 2018
Chanzo: mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Kamati Kuu ya Chadema itakutana kesho Oktoba 17,2018 kwenye kikao cha dharura cha kamati kuu ya chama jijini Dar es Salaam.
Taarifa iliyotolewa leo Oktoba 16, 2018 na Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema imeeleza kikao kitakuwa na agenda kuu ya kujadili na kuazimia kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea ndani na nje ya chama .
“Tutatoa taarifa rasmi juu ya maazimio ya kikao hiki kitakapomalizika,” amesema Mrema katikia taarifa hiyo
Chanzo: mwananchi.co.tz