Kamati kuu ya CCM Taifa iliyoketi leo mjini Dodoma chini ya Mmwenyekiti na Rais Samia Suluhu imempitisha Emmanuel Cherehani kuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Ushetu mkoani Shinyanga katika uchaguzi mdogo baada ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo ambae pia alikua Waziri wa Ulinzi Elias Kwandikwa kufariki Dunia
Pia, Kamati kuu ya chama cha Mapinduzi CCM Taifa imempitisha Mbarouk Habibu ameteuliwa kuwa mgombea jimbo la Konde
Jimbo la ushetu lilibaki wazi baada ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Elias Kwandika kufariki dunia, huku jimbo la Konde likiwa wazi mara baada ya Mbunge wake,Sheha Mpemba Faki kujiudhulu nafasi hiyo.