Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Joseph Selasini; Ni Muongo au msahaulifu?

JOESPH SELASINI ML Joseph Selasini

Fri, 1 Jul 2022 Chanzo: Mwanahalisi

ALIYEKUWA mbunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), katika jimbo la Rombo, mkoani Kilimanjaro, Joseph Selasini, ameibuka upya na kudai kuwapo mkakati unaosukwa na waliokuwa “marafiki zake,” mimi nikiwamo, kumchafua na kumvunjia hadhi yake mbele ya jamii.

Anasema, mgogoro wa uongozi unaofukuta ndani ya NCCR- Mageuzi, kwa kiasi kikubwa, unachochewa na hatua ya baadhi yetu, kutumiwa na mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia.

Alisema, “…najua kabisa, najua ndiyo maana namuambia Mbatia, amwambie Kubenea aache, kwa sababu, mimi naweza kutoa ya familia yake, kwa kuwa tunafahamiana. Hata Kubenea, naweza kutoa ya kwake pia. Ninamfahamu. Sisi tumekuwa wote kwa muda mrefu.

“Lakini mimi ni mtu mzima, nakwenda kwa hoja. Mimi siendi kwa mambo ya Kiswahili. Yaani watu wanachukulia vitu kwa mambo ya mtaani, katika mambo mazito. Siyo sahihi kusema kuwa huyu hastahili katika jamii, kwa kuwa ni mhuni, ili nini? Sisi tunaangalia nini analeta, si uhusiano wake,” alieleza.

Msingi wa madai ya Selasini, ni taarifa zinazoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari, zikimnukuu Dk. Masumbuko Lamwai, mmoja wa wanawazuoni mashuhuri nchini, akielezea maisha ya Selasini, mwenendo wake, tabia zake na hulka yake.

Dk. Lamwai, aliyekuwa mhadhiri mwandamizi wa Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), mbunge wa Ubungo na Mkurugenzi wa Katiba na Sheria (NCCR-Mageuzi), ameeleza mengi kuhusu mwanasiasa huyu.

Aidha, Dk. Lamwai, aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Dar es Salaam, diwani wa kwanza wa upinzani katika Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam, kupitia kata ya Manzese na baadaye Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, na Joseph Roman Selasini Shao, ni watoto wa Mzee Roman Selasini na mkewe, Katharine Shao.

Chanzo: Mwanahalisi