Tue, 4 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bunge limeidhinisha Wenyeviti wapya wa Bunge, ambao ni David Kihenzile Mbunge wa Mufindi Kusini, Daniel Sillo Mbunge wa Babati Vijijini, na Najma Murtaza Giga Mbunge wa Viti Maalum.
Hatua hii inatokana na Kamati ya Uongozi ya Bunge kuteua na kupendekeza majina hayo na kuyafikisha Bungeni leo Aprili 4 katika Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kumi na Moja, ili yaidhinishwe.
Hatua hiyo imetokana na kuvunjwa kwa kamati za Bunge ambapo kanuni za Bunge zinaelekeza kuteua upya wenyeviti wa Bunge.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live