Tue, 21 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo, ameitaka Serikali kuwa na tamaduni ya kufatilia fedha za umma pindi zinapopelekwa kwenye miradi mbalimbali.
Shigongo ameyasema hayo jana Juni 20, 2022 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa anachangia Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2022-23.
Amesema, fedha zinazopelekwa kwenye miradi hazifatiliwi, ndio maana zimekuwa zikiliwa na wajanja hususan kwenye halmashauri.
"Mheshimiwa Spika halmashauri ni mchwa wa fedha za umma, tumeona mheshimwa Awesu akitaka aoneshwe bwawa kule Tanga, tumeona Waziri Mkuu akizungumza pesa kutumika vibaya Msd," alisema Shigongo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live