Tue, 24 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wabunge Josephat Gwajima (Kawe) na Jerry Silaa (Ukonga) ambao ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge wameondolewa kwenye kamati hiyo hadi itakapoamuliwa vinginevyo.
Wabunge hao wameitwa mbele ya kamati hiyo wakituhumiwa kusema uongo, kushusha hadhi na heshima ya Bunge, jambo ambalo kwa mujibu wa kanuni za kamati hiyo, moja kwa moja wanakuwa wamepoteza sifa za kuwa wajumbe.
Gwajima alianza kuhojiwa jana na kamati hiyo kwa zaidi ya saa mbili na ataendelea kuhojiwa tena hii leo huku Slaa nae akitarajiwa kuhojiwa pia hii leo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live