Mon, 29 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Manota amepokelewa leo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba wakati wa ufunguzi wa kampeni za jimbo la Kinondoni zilizofanyika viwanja wa Biafra, jijini Dar es salaam.
Diwani huyo ametambulishwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba na kukabidhiwa kadi papo hapo na kuomba kukubaliwa kuingia CCM huku akiomba radhi kwa wana CCM kumsamehe kama aliwahi kuwakosea.
Hata hivyo viongozi wa Chama Chama waliokuwepo walimkaribisha diwani huyo kwa furaha na kumkaribisha rasmi CCM.