Wanachama wa Chama cha ACT-Wazalendo wamehimizwa kudumisha umoja, mshikamano na upendo miongoni mwao ili chama hicho kupata mafanikio.
Ushauri huyo umetolewa na Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Taifa, Juma Duni Haji wakati alipokuwa anazungumza kwenye kikao cha ndani na wanachama wa ACT Mkoa wa Lindi kilichofanyika ukumbi wa MM Hotel.
Duni amesema ili chama kiweze kufikia malengo wanachama hawabudi kujenga umoja na mshikamano na endapo wana ACT-Wazalendo hawatashikamana katika ujenzi na uimarishaji wa chama chao ipo hatari ya mamluki kuingia miongoni mwao, na kuwavuruga kwa lengo la kuharibu umoja na,mshikamano wao.
Amesema kuwa uongozi wa chama umejipanga kuhakikisha chama kina imarika, lakini hayo hayataweza kukamilika kama wanachama hawatakuwa na moyo wa umoja na mshikamano
"Uongozi umejipanga kujenga chama na kupiga kelele kupata tume huru ya uchaguzi na katiba mpya hivyo wanachama wana wajibu wa kujenga umoja na mshikamano" amesema Duni
Amewataka wanachama wa ACT-Wazalendo kujiunga uanachama kwa njia ya kidigitali ili kurahisisha ukusanyaji mapato na utoaji huduma ikiwemo uhakiki wa wanachama.
Advertisement Kwa upande wake mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Kanda ya Kusini, Selemani Bungara amesema kuwa kanda ya kusini wako imara wanajipanga kuhakikisha chama kinasonga mbele.