Dk. Nchimbi awahakikishia wana CCM kuwa Chama kitaendelea kuimarisha usimamizi wa serikali zake kuhakikisha kwamba serikali zinatimiza wajibu wake wa kutekeleza ilani ya CCM na kuwatumikia wananchi kwa uadilifu mkubwa.
Alisema, kazi wanazozifanya marasi Dk. Samia na Dk. Mwinyi ni kubwa na kwamba inahitaji wanaCCM kupitia chama chao kuimarisha usimamizi wa serikali hizo, na kuwahakikishia watazisimamia serikali chini ya Mwenyekiti wa CCM.
Aidha aliwakumbusha wana CCM juu ya kuvunja makundi kipindi ambacho uchaguzi unamalizika na kupatikana kiongozi aliyechaguliwa na wote wanatakiwa kumuunga mkono kiongozi huyo.