Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dk Bashiru awaonya wanasiasa waropokaji

65918 Pic+bashiru

Mon, 8 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Siha. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Bashiru Ally amewaonya wanasiasa nchini Tanzania kuachana na tabia ya kuropoka maneno yanayoweza kuhatarisha usalama wa Taifa.

Ametoa kauli hiyo jana Jumapili Julai 7, 2019 katika kikao cha ndani kilichofanyika Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro na kuwahusisha viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama hicho tawala nchini Tanzania.

Dk Bashiru aliyepo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya siku nne amesema wanasiasa wakianza kuropoka nchi itapotea.

“Mtu akiropoka mnamjibu palepale ili kutuliza hali ya hewa kwa sababu waropokaji hawapo Kenya peke yake na Tanzania wapo,” amesema Dk Bashiru akitolea mfano kauli isiyofaa iliyotolewa hivi karibuni na mwanasiasa mmoja nchini Kenya.

Alitumia nafasi hiyo kuwataka viongozi wa chama na Serikali kuwa makini na taarifa za upotoshaji, kutoamini kila taarifa wanayoiona mitandaoni.

Chanzo: mwananchi.co.tz