Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dk Bashiru ataka wana CCM kuwaheshimu wapinzani

48207 Bashirupic

Sat, 23 Mar 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Bashiru Ally amewataka wanachama wa CCM kutobeza na badala yake kuheshimu alama za vyama vyote vya siasa nchini kwa sababu vimesajiliwa kisheria.

Dk Bashiru amesema hayo leo Jumamosi Machi 23, 2019, wakati akizindua mkakati wa kukomaza demokrasia kwenye mashina ulioandaliwa na CCM mkoa wa Dodoma.

Amewataka kutochoma wala kubeza alama za vyama hivyo na kwamba hivi karibuni kuna wafuasi wamechoma bendera na kupaka rangi ya chama chao ofisi za chama kingine.

"Ni kosa kuparamia na kupaka rangi ofisi za vyama hivyo. CCM tusifanye hivyo ni kosa kisheria. CCM tusifanye holela na uhuni huo katika siasa," amesema.

Ametaka wanachama wa CCM kuwa mfano bora na kwamba Serikali ina wajibu wa kulinda vyama vyote vilivyosajiliwa kisheria.

 



Chanzo: mwananchi.co.tz