Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dk Bashiru: Sijafurahia utendaji wa mkurugenzi Wilaya ya Rombo

66343 Bashirupic

Wed, 10 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Same. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Dk Bashiru Ally amesema utendaji kazi wa mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Rombo, Magreth John haujamfurahisha.

Ametoa kauli hiyo leo Jumatano Julai 10, 2019 wakati akizungumza kwenye kikao kilichofanyika katika jimbo la Same Mashariki na kuwakutanisha viongozi wa chama hicho tawala na Serikali ya Tanzania.

"Jana nilikuwa Rombo mkurugenzi hakunifurahisha nimeacha ujumbe ajifunze kwa wenzake kwa kuwa natambua wanawake viongozi Kilimanjaro wanachapa kazi na mko vizuri lakini msibweteke.”

"Katika Mkoa wa Kilimanjaro tunao viongozi wanawake, mkuu wa Mkoa, wakuu wa wilaya, katibu wetu wa wilaya ni mwanamke na pia kuna wabunge watatu wanawake na wote wameniridhisha yule wa Rombo ni mwanamke ila hajanifurahisha,” amesema Bashiru.

Amewataka viongozi wanawake kusimamia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa kuwa utendaji wao ni mzuri.

Dk Bashiru pia amewaonya watumishi wa chama hicho wanaotumia magari ya chama katika shughuli binafsi, kwamba watakaobainika hawatavumiliwa.

Pia Soma

 

 

Chanzo: mwananchi.co.tz