Katibu Mkuu wa Chama cha mapinduzi CCM Dkt. Bashiru Ally amewakumbusha wana CCM kutambua kuwa uteuzi utakaofanywa kwa wagombea utazingatia kanuni na misingi iliyowekwa na chama hicho.
Katibu Mkuu wa Chama cha mapinduzi CCM Dkt. Bashiru Ally amewakumbusha wana CCM kutambua kuwa uteuzi utakaofanywa kwa wagombea utazingatia kanuni na misingi iliyowekwa na chama hicho. Dk Bashiru ameyabainisha hayo huko jijini Dodoma na kuongeza kwa kusema kuwa uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa umewataka watia nia wote waliogombea Ubunge wa majimbo na wale wa viti maalum, kukaa katika majimbo yao, wakisubiri uteuzi kwa wale watakaogombea kupitia chama hicho.