Katibu mkuu wa Chama cha Mapindizi (CCM) Daniel Chongolo ametaka Maoni ya Wananchi kuhusiana na Mjadala wa Uwekezaji na Uendelezaji wa Bandari yaanze kukusanywa, ambapo yale ambayo yataonekana kuwa na tija ndio yatakayofanyiwa kazi.
Komredi Daniel Chongolo ametoka Kauli hiyo leo Wilayani Korogwe mkoani Tanga katika mkutano wake wa Hadhara wakati alipokuwa akielezea usahihi wa Makubaliano ya Mkataba wa Uwekezaji wa Bandari hapa nchini.
"Sisi tumesema maoni ya Wananchi yakusanywe, yale yenye tija yaingizwe kwenye Mjadala na Kwenye mkataba utakaoingiwa kwa ajili ya Uendeshaji wa Bandari au Sehemu ya Bandari yetu" amesema Chongolo.