Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chauma), Hashimu Rungwe amesema licha ya changamoto mbalimbali ikiwamo ya kuzuiliwa mikutano ya hadhara, chama hicho hakitasusia uchaguzi ujao wa Serikali za mitaa.
Amesema uchaguzi huo ni muhimu hivyo kama wataususia, watawanyima haki wananchi ya kupata viongozi bora na wanaowahitaji.
Rungwe ameyasema hayo leo Jumapili Oktoba 20, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari akilenga kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura.
“Sisi hatutasusia na wala hatuna mpango huo kwa sababu huu ni uchaguzi muhimu sana kwa wananchi na si wa mtu binafsi wala chama binafsi, hivyo kila chama kina haki ya kushiriki kwa kuwa kinatambulika katika ofisi ya msajili wa vyama,” amesema Rungwe.
Amesema chama hicho kimejipanga kuweka mgombea kila mtaa katika mikoa yote nchini.
“Mapema Oktoba 29, wagombea wetu wataenda kuchukua fomu wajaze na kuzirejesha ili michakato mingine iendelee, kwa hiyo tunaomba wajitokeze kwa wingi kuwania nafasi hizo hasa wanawake,” amesema mwenyekiti huyo.
Pia Soma
- LIVE: IBADA YA UPEPO WA KISULISULI MLIMA WA MOTO, MAMIA WAJITOKEZA
- Hillary aibua madai mengine ya Urusi kutaka kumsaidia Trump
- Upepo wa kisulisuli wavuta wengi Kanisa la Mlima wa Moto, vijana kibao wajitokeza