Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Chadema Arumeru washtushwa Nassari kung’olewa ubunge

46851 Pic+nassari

Fri, 15 Mar 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arumeru. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Jimbo la Arumeru Mashariki kimeeleza kupokea kwa mshtuko taarifa za kuvuliwa ubunge, Joshua Nassari na Spika wa Bunge, Job Ndugai na kimewataka wanachama wake kutulia wakati suala hilo linashughulikiwa kisheria.

Soma zaidi: Alichokisema Joshua Nassari baada ya kuvuliwa ubunge

Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Meru, Gadiel Mwanda amesema sababu zilizotolewa na Spika kuwa Nassari ameondolewa kwa kutohudhuria vikao vitatu mfululizo bila taarifa zimewaumiza wengi.

"Suala hill limepokelewa katika mitazamo tofauti, wapo walioumia kwa kuamini kuwa Mhe Nassari anaonewa kwa kuhukumiwa pasipo kupewa nafasi ya kusikilizwa huku wakiamini kuwa alitoa taarifa kwa barua aliyoituma kwa Spika kupitia Email rasmi ya Bunge Februari 29, 2019. Lakini wapo walioumia kwa kuamini kuwa alifanya uzembe," amesema.

Soma zaidi: Joshua Nassari apoteza sifa ya kuwa mbunge

Amesema Chadema jimbo la Arumeru Mashariki inawapa pole wanachama  wote na wananchi kwa ujumla kwa lililotokea na kwamba inawasihi kuwa watulivu,wastahimilivu na wakomavu katika kipindi hiki kigumu.

Mwanda amesema Chadema Jimbo kwa kushirikiana na Nassari Mbunge wana fanya mawasiliano na uongozi wa Chama Taifa pamoja na wanasheria  kwa mashauriano na baada ya hapo watawafahamisha rasmi muda na mahali ambapo Mhe,Nassari na uongozi wa Chama watafanya mkutano na vyombo vya habari



Chanzo: mwananchi.co.tz