Dar es Salaam. Mwezi mmoja kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa ubunge jimbo la Buyungu na Kata 79, vyama vya Chadema na ACT-Wazalendo vimeanza mazungumzo ya kushirikiana katika uchaguzi huo utakaofanyika Agosti 12, 2018.
Mazungumzo hayo yamefanyika leo Ijumaa Julai 13, 2018 jijini Dar es Salaam, huku ACT ikiwakilishwa na Omar Said Shaaban ambaye pia ni rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS).
Timu ya Chadema katika mazungumzo hayo imeongozwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi, Oganaizesheni na Uchaguzi,
Akizungumza na MCL Digital, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu amesema baada ya kumalizika kwa mazungumzo wamewaachia jukumu Chadema kwenda kujadiliana.
“Tulichokizungumza wenzetu wa Chadema wanayajadili katika ngazi ya sekretarieti kabla ya kufanya makubaliano ya mwisho. Hekima inatutaka kuwasubiri wenzetu wajadiliane, waafikiane na kisha tufanye makubaliano ya mwisho. Tunasubiri,” amesema Shaibu