Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

CHADEMA wagoma kukutanishwa na jeshi la polisi

Wakataa1 CHADEMA wakataa kukutanishwa na Polisi

Tue, 7 Sep 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema hakipo tayari kukutanishwa na jeshi la polisi, kama ambavyo ametangaza Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi ili kuondoa mvutano kati yao, vyama vya siasa na jeshi hilo.

Hayo yamesemwa leo Jumanne Septemba, 7,2021 na Mkurugenzi wa Itikadi, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alipozungumza na waandishi wa habari.

Mrema amesema hawaoni haja ya kukutanishwa na jeshi hilo kwa kuwa kwa mambo ambayo wamekuwa wakiyafanya kwa miaka sita amedai ni wahalifu ambao wangetakiwa wawe wameshafikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live