Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

CCM yatakiwa kujitathimi kwa wanaokimbizana nao

Ccmpicmm CCM yatakiwa kujitathimi kwa wanaokimbizana nao

Thu, 10 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwaka 1995 katika Mkutano Mkuu wa CCM, Baba wa Taifa Julius Nyerere alisema bila CCM, imara nchi itayumba kwa kuwa Watanzania wanataka mabadiliko na wasipoyaona au kuyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya chama hicho.

Wakati huo Mwalimu Nyerere akitoa kauli hiyo vyama vya upinzani vilikuwa na miaka mitatu tangu vianzishwe. tangu wakati huo mpaka sasa vyama hivyo vimechagiza ukuaji wa demokrasia na kutoa upinzani mkali kwa CCM ambao kwa namna moja au nyingine umekimarisha chama hicho kikongwe.

Usijisifu kwa kuwa na mbio bali msifu pia anayekukimbiza! ndivyo unavyoweza kusema baada ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kutambulisha kadi za kieletroniki wakiingia kwenye uendeshaji wa chama kwa njia za kisasa.

CCM kimetimiza miaka 45 kikiwa madarakani, si miaka michache lakini kinapojisifia kwa uimara wake ni lazima kiangalie na wanaokikimbiza mpaka kikapata mafanikio iliyonayo hivi sasa.

Mfumo wa vyama vingi vya siasa uliorejea nchini mwaka 1992 na mwaka 1995 kushuhudiwa uchaguzi mkuu wa kwanza uliohusisha vyama vingi umechangia kuimarika kwa chama tawala.

CCM haiwezi kuwa imara kama vyama vya upinzani si imra kwakuwa vyenyewe ndivyo huonyesha udhaifu wa chama tawala kwa wananchi ili navyo vipate uungwaji mkono

Tayari baadhi ya vyama vya upinzani viliaanza kuingia katika matumizi ya teknolojia ya kisasa kwenye uendeshaji wake. Ni zama za kidijitali hivyo vyama vya siasa hapa nchini haviwezi kukwepa matumizi ya mifumo ya kisasa ambayo si tu inaboresha shughuli zao lakini pia inawapa fursa ya kutambulika zaidi nje ya mipaka ya Tanzania.

Vyama hivyo hivi sasa vinaona fursa ya kusajili wanachama, kupokea michango ya wanachama, kutunza kumbukumbu, kutoa kadi za kieletroniki na kutoa taarifa mbalimbali kuhusu maendeleo, programu na mikutano ya chama husika.

Kimsingi vyama vya siasa zinaweza kutumia mifumo ya kisasa kujiendesha kupitia ada na michango mbalimbali inayotolewa na wanachama, marafiki, wafadhili na wahisani.

Mifumo ya kieletroniki ni njia mojawapo wa kudhibiti ubadhirifu, ukosefu wa taarifa sahihi za wanachama na uhifadhi hafifu wa nyaraka za chama.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live