Mon, 21 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimefuta uchaguzi wa Umoja wa Vijana mkoa wa Simiyu na kusimamisha uchaguzi wa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kwa mikoa ya Arusha na Mbeya.
Sababu za kufanya hivyo ni kutokana na tuhuma za rushwa katika chaguzi hizo huku uchaguzi wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi kuhusu tuhuma za kada kubeba boksi la kura ukichunguzwa.
Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo ametangaza hayo leo Jumatatu Novemba 2022 huku akisema kuwa chama hakitavulimia kuwa na viongozi wanaotuhumiwa au kujihusisha kwa rushwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live