Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza, leo Jumamosi Juni 25, 2022 kimetangaza kuanza kutoa fomu za kugombea nafasi ya makamu mwenyekiti wa halmashauri za wilaya.
Uchaguzi wa nafasi hiyo utafanyika Julai 2022.
Katibu wa CCM wilaya ya Sengerema, Mhusini Zikatimu amesema hadi sasa Maxmiliani Mkugungu ambaye ni makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Buchosa amechukua fomu ya kutetea nafasi hiyo.
Amewataka madiwani wengine wajitokeze kuchukuwa fomu kutokana na chama hicho kuwa Demokrasia ya kweli ya kupata viongozi wake, ameeleza kesho Jumapili ni siku ya mwisho kuchukua fomu.