Sun, 28 Jul 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Bukoba. Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania kimeanza kuimarisha mikakati yake kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa kuzindua kampeni ya Kagera ya kijani.
Uzinduzi huo unafanyika leo Jumamosi Julai 27, 2019 katika viwanja vya Hamugembe mjini Bukoba ambako wanachama na viongozi kutoka wilaya zote za Mkoa wa Kagera wanaendelea kuwasili.
Pia uzinduzi huo unaoratibiwa na Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kagera unatarajiwa kuwakusanya baadhi ya vigogo wa chama hicho wakiwemo wabunge na makada maarufu kutoka mikoa jirani.
Chanzo: mwananchi.co.tz