Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

CCM wapita bila kupingwa vijiji 6,248

83698 Pic+ccm CCM wapita bila kupingwa vijiji 6,248

Thu, 14 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Selemani Jafo amesema wagombea 6,248 kati ya 12,319 wanaotokana na Chama cha CCM wamepita bila kupingwa baada ya kutojitokeza kwa wagombea wa vyama vingine.

Akizungumza leo Jumapili Novemba 10, 2019, Jafo amesema pia wagombea uwenyekiti wa chama hicho 1,169  kati ya mitaa 4,263 sawa na asilimia 27 wamepita bila kupingwa.

“Kwa upande wa vitongoji Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika vitongoji 37,505 kati ya vitongoji 64,384 sawa na asilimia 58,” amesema.

Amesema katika wajumbe wa kundi la wanawake jumla ya wajumbe 64,085 wamepita bila kupingwa na wajumbe kundi la mchanganyiko jumla ya wajumbe 75,560 wamepita bila kupingwa.

Chanzo: mwananchi.co.tz