Fri, 10 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM Ndg. Faki Raphael Lulandala (Mnec) akiwa Mkoani Njombe amekutana na kuzungumza na Vijana wanaojitegemea kwa shughuli ya Bodaboda kufahamu kero na changamoto zao.
Aidha Katibu Mkuu amewaeleza boda boda wa Mkoa wa Njombe “Chama cha mapinduzi kina itambua ajira yenu ya boda boda, hii ni kazi rasmi kama zilivyo kazi nyingine”.
Sambamba na hilo amewapongeza UVCCM Njombe chini ya Mwenyekiti wake Ndg. Samweli Mgaya kwa kuwajengea Vijana wa Bodaboda Vituo vinavyowakinga wakati wa Mvua na Jua kali.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live