Mon, 19 Jul 2021
Chanzo: globalpublishers.co.tz
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeshinda uchaguzi katika jimbo la Konde visiwani Zanzibar, baada ya mgombea wake Sheha Faki kujipatia kura 1,796 na kuwashinda wagombea wenzake 11.
Matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika jana Jumapili, Julai 18, 2021 yametangazwa leo Julai 19, 2021, ambapo Faki amepata kura 1,796 kati ya kura halali 5,020 zilizopigwa.
Uchaguzi huo mdogo umefanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kutokea Chama cha ACT-Wazalendo Khatib Said, kufariki dunia Mei 19 mwaka huu.
Chanzo: globalpublishers.co.tz