Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

CCM Pwani watoa tamko Ndugai kuomba radhi

Cccm Picha Data CCM Pwani watoa tamko Ndugai kuomba radhi

Tue, 4 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kimesema kitendo cha Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kujitokeza hadharani na kukiri mapungufu na kutoa ufafanuzi kuhusu kauli yake juu ya suala la mikopo ya nchi na kuleta taharuki, sio kujidhalilisha bali kujiimarisha.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha leo Jumanne Januari 4, 2021 Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo, Ramadhani Meneno amesema kitendo hicho cha Spika Ndugai kijitokeza hadharani chama kinaamini ni cha kijasiri na kiungwana .

"Kitendo cha Spika Ndugai kujitokeza hadharani na kuomba radhi kwa Rais Samia na Watanzania ni cha kijasiri na kiungwana hivyo ombi langu kwa wana CCM wenzangu na Watanzania kuiamini kauli yake  " amesema na kuongeza

"Nampongeza sana Spika Ndugai kwa uungwana wake kwani hivyo ndivyo tulivyolelewa na Chama chetu" ameongeza Maneno.

Jana Jumatatu Januari 3, 2022 Spika Ndugai alijitokeza hadharani na kumuomba radhi Rais Samia Suluhu Hassan na Watanzania kama hotuba yake aliyoitoa hivi karibuni ilimvunja moyo Rais.

SOMA ZAIDI: Ndugai amuomba radhi Rais Samia, Watanzania

Advertisement Ndugai alisema hotuba yake haikuwa na jambo la kukashifu wala kudharau juhudi za Serikali bali alikua anasisitiza ulipaji wa kodi na tozo mbalimbali.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live