Tue, 27 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amesema kilichopitishwa na bunge sio mkataba, ni makubaliano ambayo ni hatua ya kuelekea kwenye mkataba.
Amesema kuwa makubaliano hayo hayawezi kusema muda kwa sababu unazungumzia ushirikiano baina ya nchi mbili ambayo yanaweka msingi wa majadiliano ambayo yatapelekea mikataba, hivyo huwezi kuweka muda kwenye kitu ambacho hamjajadiliana na kukubaliana.
Aidha, amesema makubaliano hayo hayamaanishi kwamba mwekezaji atapewa bandari zote na kwamba akija mwekezaji mwingine mwenye dau kubwa zaidi, wanaweza kumpa mwingine.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live