Chama cha ACT-Wazalendo kimemtangaza mwanasiasa Hamidu Bobali aliyekuwa Mweyekiti wa Jumuiya ya vijana CUF, (JUVICUF), na Mbunge wa Mchinga kuwa Mwanachama mpya wa chama hiko.
Chama cha ACT-Wazalendo kimemtangaza mwanasiasa Hamidu Bobali aliyekuwa Mweyekiti wa Jumuiya ya vijana CUF, (JUVICUF), na Mbunge wa Mchinga kuwa Mwanachama mpya wa chama hiko. Akizungumza wakati wa kumtambulisha mwanachama huyo mpya, Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu amesema hatua hiyo ni kufuatia awamu ya pili ya Oparesheni Shusha Tanga, Pandisha Tanga ambayo inadhamiria kupokea wanachama wapya kutoka katika vyama mbalimbali.