Bashungwa ameahidi kuwa Wizara yake itahakikisha inaendelea kutoa ushirikiano wa dhati kwa viongozi waliochaguliwa ili kuimarisha sekta ya michezo bungeni ili kuhakikisha klabu hiyo inafanya vizuri kwa kipindi chote.
Viongozi waliochaguliwa ni pamoja na Abbas Tarimba ambaye amechaguliwa kuwa Mwenyekiti, Esther Matiko ni Makamu Mwenyekiti na Seif Gulamali ni Meneja wa Klabu, nafasi tano za Kamati ya Utendaji zimechukuliwa na Ridhiwani Kikwete, Anna Lupembe, Rose Tweve , Aishi Hillaly na Stanslaus Mabula.
Aidha, Bashungwa amewashukuru Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanikisha zoezi la uchaguzi wa viongozi hao lililofanyika Jana Aprili 12, mwaka huu