Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Baada ya CHADEMA, NCCR Mageuzi nao wanena

68509 Mbatia+pic Baada ya CHADEMA, NCCR Mageuzi nao wanena

Thu, 4 Jun 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Baada ya CHADEMA, kuwataka watangaza nia ya kugombea nafasi ya Urais ndani ya chama hicho wajitokeze, NCCR Mageuzi nao wamesema kuwa wanatarajia kutoa ratiba ya uteuzi wa wagombea Urais, Ubunge na Madiwani juma lijalo, na kuiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutenda haki katika uchaguzi ujao.

Hayo yamebainishwa leo Juni 4, 2020, na Mwenyekiti wa chama hicho James Mbatia, Jijini Dodoma na kusema kuwa kwa sasa kimefungua milango kwa vyama vingine vya siasa nchini, ambavyo vipo tayari kushirikiana ili kuiondoa Serikali ya Chama cha Mapinduzi madarakani.

Aidha Mbatia amezungumzia kuhusu mlipuko wa Virusi vya Corona na kuwaomba wananchi kuendelea kuchukua tahadhari zaidi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live