Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

BREAKING: Rais Magufuli apitishwa kugombea tena CCM baada ya Tafakuri ya kina

297 Screen Shot 2017 12 17 At 4.28.34 PM 660x400.png TZW

Sun, 17 Dec 2017 Chanzo: millardayo.com

Ni kutoka Dodoma leo December 17, 2017 ambapo Katibu wa Itikadi na uenezi CCM Humphrey Polepole ametangaza maamuzi mapya ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM.

Namnukuu Polepole akisema “Baada ya tafakuri ya kina, Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kimeazimia kwa kauli moja kuwateua na kuwapitisha wafuatao, wa kwanza Dr. John Pombe Magufuli kusimama na kugombea nafasi ya Mwenyekiti CCM“

“Wa pili ni Dr. Ally Mohamed Shein kusimama na kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, wa tatu ni Philiph Mangula kusimama na kugombea nafasi ya Makamu wa Mwenyekiti wa CCM bara” 

Tazama mengine zaidi yaliyosemwa na Humphrey Polepole kwenye hii video hapa chini

“CHADEMA WAACHE KIKI, WAMEANZA KUCHANGANYIKIWA” – MBUNGE MUNDE

Chanzo: millardayo.com