Wed, 24 Jan 2024
Chanzo: Mwananchi
Mtu mmoja ambaye jina lake halijafahamika ameishiwa nguvu wakati maandamano ya wafuasi wa Chadema yakiendelea kuelekea ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo Barabara ya Sum Nujoma jijini Dar es Salaam leo Januari 24, 2024.
Mtu huyo alipoteza nguvu na kusaidiwa na waandamanaji wenzake waliokuwa pamoja naye na kumpeleka kivulini kisha kumlaza na kuanza kumpepea.
Maandamano hayo tayari yamefika ofisi za UN ambapo viongozi wa Chadema wameingia ndani kuwasilisha barua yenye ujumbe wanaoukusudia.
Chanzo: Mwananchi