Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Afande Sele atangaza kujiunga na CCM, Aeleza sababu

4830 Capture 43 TZW

Sat, 17 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Rapa mkongwe nchini Tanzania, Afande Sele ametangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi leo Machi 15, 2018 mkoani Morogoro mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Afande Sele

Afande Sele amesema sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli katika kupambana na rushwa na kuwajali wanyonge.

Hata hivyo, Mfalme huyo wa Rhymes amewaomba wanachama wa Chama cha Mapinduzi wampokee kwa mikono miwili.

Afande Sele kabla ya kujiunga na CCM alishawahi kuwa mwanachama wa CHADEMA na Chama cha ACT Wazalendo ambapo mwaka 2015 alitangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Morogoro Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo.

Rais Magufuli leo Machi 15, 2018 amezindua kiwanda cha kutengeneza sigara cha Philips Moris International mjini Morogoro ambapo Afande Sele alitumia nafasi hiyo kujiunga na CCM.

 

Chanzo: bongo5.com