Mon, 8 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
CHAMA cha ACT Wazalendo Mkoa wa Njombe kimetangaza kushiriki uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Njombe mjini utakapotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutokana na nafasi hiyo kuwa wazi baada ya aliyekuwa Diwani Romanus Mayemba, kufariki dunia.
:
“Kuzira uchaguzi ni kukiuka katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwasababu katiba inatambua ushiriki wa vyama vya siasa kwenye uchaguzi na kushindana kwa hoja.”amesema Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo mkoani Njombe Ally Mhagama (Dk. Sagasaga)
Chanzo: www.tanzaniaweb.live