Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

12 wajitosa kumrithi Lissu

67165 Lissupic

Wed, 17 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Singida. Wagombea 12 wa vyama vya siasa nchini Tanzania wamejitokeza kuchukua fomu kuomba kuteuliwa kuwania  ubunge wa Singida Mashariki kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Tundu Lissu.

Uchaguzi mdogo katika jimbo hilo utafanyika Julai 31, 2019 na tayari uchukuaji na urejeshaji fomu umeanza ukitarajiwa kuhitimishwa kesho Alhamisi Julai 18, 2019.

Kesho pia utafanyika uteuzi wa wagombea na Ijumaa Julai 19 hadi Julai 30, 2019 ni muda wa watakaopitishwa kufanya kampeni.

Msimamizi wa uchaguzi huo, Justice Kijaji amelieleza Mwananchi jana kuwa waliochukua fomu na vyama vyao katika mabano ni;

Hamidu Hussein (ADA-Thadea), Tirubya Mwanga (UPDP), Ameni Npondia (CCK), Amina Ramadhan (DP) na Ayuni John (UDP).

Wengine ni Amina Mcheka (AAF), Maulid Mustafa (ADC), Selemani Ntandu (CUF), Feruzy Fenezyson (NRA), Abdallah Tumbo (UMD), Donald Mwanga (TLP) na Masalio Kyara (SAU).

Pia Soma

Mgombea wa CCM, Miraji Mtaturu anatarajiwa kuchukua fomu leo.

Uchaguzi huo unafanyika baada ya Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kutangaza Lissu kupoteza sifa ya kuwa mbunge kutokana na kutojaza fomu za mali na madeni ya viongozi wa umma na kutotoa  taarifa ya mahali alipo.

Spika Ndugai aliitaka Tume ya Taifa  ya Uchaguzi (NEC) kuendelea na mchakato wa kujaza nafasi hiyo.

Lissu amekuwa nje ya Tanzania tangu Septemba 7, 2017 akitibu majeraha ya risasi 16  alizomiminiwa akiwa katika makazi yake Area D jijini Dodoma akitoka kuhudhuria kikao cha Bunge kilichokuwa kikiendelea.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz