Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Zifahamu faida za kula mboga ya Sukuma Wiki

Aukuma Wiki.jpeg Zifahamu faida za kula mboga ya Sukuma Wiki

Mon, 2 Jan 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Sukuma wiki ni mboga maarufu katika nchi za Afrika Mashariki na watu wengi huitumia kila siku.

Kuna sababu kuu mbili za mboga ya sukuma wiki kuliwa zaidi nchini Kenya.

Mwanzo, sukuma wiki tofauti na mboga nyingine, hupandwa kila sehemu nchini na pia inaweza kustawi katika maeneo ya ukame kupitia umwagiliaji wa maji.

Pili, sukuma wiki ndiyo mboga yenye bei nafuu zaidi nchini Kenya na inauzwa kwa bei ya chini kuanzia KSh5 na kuifanya kuwa chakula kinacholiwa zaidi.

Hata hivyo, jambo ambalo Wakenya wengi hawana habari ni kwamba kuna hatari zinazohusiana na ulaji wa sukuma wiki kila siku;

1. Kemikali zenye madhara

Mboga nyingi za sukuma wiki zina kemikali hatari kulingana na utafiti uliochapishwa na Kenya Organic Agriculture Network (KOAN, 2021)

Utafiti huo ulifichua kuwa kati ya sampuli 10 za sukuma wiki zilizochunguzwa nchini Kenya, tisa zilikuwa na asilimia 90 ya viuatilifu vyenye sumu.

Kwa mujibu wa utafiti huo, kemikali hizo zinatokana na matumizi mabaya ya dawa, ukosefu wa usafi wa hali ya juu sokoni, na uchafu wakati wa kupika.

2. Kuvimba tumbo

Kwa mujibu wa ripoti ya Medical News Today (2022), sukuma wiki inaweza kusababisha tumbo kuvimba kwa watu ambao wana ugumu wa kusaga chakula.

FODMAPs inasema wanga zenye mnyororo mfupi ni sugu kwa usagaji wa chakula.

Badala ya kufyonzwa ndani ya damu yako, hufika mwisho wa utumbo wako, ambapo bakteria nyingi za utumbo hukaa.

Unaweza pia kupata shida ya utumbo kutokana na utumiaji mwingi wa sukuma wiki.

Pia soma

Mwaka wa Hustler: 2022 William Ruto Ndiye Aliafikia Mengi

Mawe ya figo na masuala mengine yanayohusiana na afya

Kulingana na Mamlaka ya Kikaboni (2022), ulaji wa Sukuma wiki kila siku unaweza kusababisha mawe kwenye figo.

"Sukuma wiki ina oxalates, kwa bahati mbaya, oxalates kwa wingi sana inaweza kuweka kwenye figo, na kusababisha malezi ya mawe. Kwa hiyo, ni bora kula mboga hii kwa kiasi,” jarida la kitiba laonya.

Faida za lishe ya Sukuma Wiki

Kando na hatari za kiafya zinazohusiana na Sukuma Wiki, mboga hizo zina faida nyingi za kiafya.

Mwanzo ni chanzo cha vitamini A ambayo huimarisha macho kuona vizuri usiku.

Sukuma wiki pia ina nyuzinyuzi, ambayo husaidia katika usagaji chakula na kupunguza viwango vya kolesteroli katika mwili wa binadamu.

Pia ina kalsiamu, ambayo ni muhimu katika malezi ya damu na mfupa kwa mtiririko huo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live