Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wiki mbili kituo Cha Afya kianze kufanya kazi - Naibu Waziri

DUGANGE (1) Wiki mbili kituo Cha Afya kianze kufanya kazi

Tue, 17 Jan 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange ameagiza viongozi wa Wilaya ya Itilima na Mkoa wa Simiyu, kuhakikisha hadi kufikia Februari 01, 2023 kituo cha Afya Mwanunda kinaanza kufanya kazi na wananchi wanapata huduma.

Kituo hicho ambacho kipo katika Wilaya hiyo, baadhi ya majengo yamekamilika ujenzi wake asilimia 100, ambapo Naibu Waziri amesema watalaamu Idara ya Afya Wilaya na Mkoa washirikiane na kuhakikisha hadi kufikia muda huo kituo kinaanza kufanya kazi.

Dkt. Dugange ametoa maagizo hayo leo alipofanya ziara ya siku moja Wilayani huyo na kutembelea ujenzi wa kituo hicho, huku akiridhishwa na ujenzi wa majengo yaliyokamilika na kueleza kuwa yanaendana na thamani ya pesa.

Amesema kuwa hadi kufikia tarehe hizo, mganga mkuu wa Wilaya na Mkoa, wahakikishe dawa zinakuwepo kwenye kituo hicho pamoja na watoa huduma ili wananchi waanze kupata huduma haraka iwezekanavyo.

Amesema kuwa ameelezwa kuwa kuchelewa kutoa huduma kwa kituo hicho inatokana na kutokamilika kwa taratibu za usajili, ambapo ameelekeza watalaamu hao kufuatilia usajili Wizara ya Afya ndani ya wiki moja.

“ Ndani ya wiki mganga mkuu wa Wilaya na wa mkoa, mshirikiane kituo kipate usajili, tumekubaliana hadi tarehe 01 Februari, 2023 wananchi waanze kupata huduma hapa, hivyo hakikisheni dawa zinakuwpo, vifaa tiba na watalaamu” amesema Dkt. Dugange.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live