Dar es Salaam. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, na Watoto nchini Tanzania, Ummy Mwalimu ametangaza wiki moja kwa ajili ya kutoa chanjo ya rubella na surua kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano katika halmashauri zote nchini humo.
Chanjo hiyo itaanza kutolewa kati ya Septemba 25 hadi 30, 2019.
Waziri huyo ameyasema hayo leo Jumatatu Septemba 9, 2019 jijini Dar es Salaam wakati akikabidhi magari 71 yaliyo na thamani ya Sh7.7 bilioni.
Magari hayo yamenunuliwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ambao ni Shirika la The Global Alliance for Vaccines and Immunisation (GAVI Alliance) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (Unicef) kwa ajili ya kuimarisha usambazaji wa chanjo ambapo 61 kati yake yameelekezwa katika halmashauri.
Amesema lengo la kutoa chanjo hizo ni kutaka kuhakikisha magonjwa hayo yanakomeshwa huku akihamasisha watu wengi zaidi kushiriki.
“Takwimu zinaonyesha kuwa dola 1 ya kimarekani itakayowekezwa katika chanjo inaokoa dola 6 za kimarekani zinazoweza kutumika katika matibabu hivyo ni vyema tukaweka nguvu nyingi katika upande huo.
Pia Soma
- Shule za Atlas zafanya maombi kuelekea mtihani darasa la saba
- VIDEO: Udom wazungumzia matokeo ya wanafunzi 8,500 kuzuiwa
- Erick Omondi, Mc Pilipili ‘kuwavunja mbavu’ wakazi wa Dodoma
- Mugabe kuzikwa Septemba 15, viongozi watakiwa kuwahi siku mbili kabla ya mazishi
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa huduma za kinga kutoka wizara ya afya, Leonard Subi amesema licha ya kutolewa kwa magari hayo katika halmashauri lakini bado yanahitajika zaidi ili kurahisisha ufikishaji wa chanjo katika sehemu husika.
“Tutaendelea kushirikiana na wadau wetu ili kuhakikisha chanjo hizi zinawafikia walengwa ndani ya wakati muafaka,” amesema Subi