Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waziri Ndugulile autaka uongozi Hospitali ya Nachingwea kurekebisha kasoro

16403 Afya+pic TanzaniaWeb

Sun, 9 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Lindi. Naibu Waziri wa Afya, Faustine Ndugulile ameutaka uongozi wa wilaya Nachingwea mkoani Lindi kukaa pamoja ili kutatua changamoto za kiutendaji zinazosababisha kukwamisha   ukarabati wa hospitali ya wilaya hiyo na vituo vya  afya.

Dk Ndugulile ameyasema hayo leo Septemba 8 alipotembelea Hospitali ya Wilaya  na kubaini utendaji usioridhisha ikiwemo utunzaji duni wa dawa, uchafu  wa mazingira na ucheleweshaji wa ukarabati wa hospitali hiyo.

“Utendaji na usimamizi mbovu wa mambo ni miongoni mwa kasoro zilizopo hapa,” amesema.

Amesema amebaini pia udhaifu katika utunzaji wa kumbukumbu za dawa na rekodi za kuingia na kutoka kwa vifaa tiba.

Amesema ingawa serikali imepeleka Sh400 kwa ajili ya ukarabati wa hospitali hiyo lakini hakuna kilichofanyika.

“Hali hii inakwamisha nia njema ya serikali  ya kuwahudumia wananchi wake ambao ndio walipa kodi na wadau wakubwa wa maendeleo na uchumi wa nchi,” amesema.

 

Pia Ndugulile ameutaka uongozi wa hospitali hiyo  kuhakikisha eneo la hospitali hiyo linakuwa  safi.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo  Samuel Laizer amesema kuchelewesha kwa ukarabati wa hospitali kumetokana na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri kuwa na urasimu.

“Nimejaribu kumshauri zaidi ya mara mbili kwa maandishi lakini amekuwa akiendelea na msimamo wake na kudai kwamba anatafuta mkandarasi mwenye uwezo ,” amesema

 

 

Chanzo: mwananchi.co.tz